Millionaire  Ads

Thursday, November 17, 2016

Hamilton kutwaa Ubingwa?

Tags

Nguli ampa tano Hamilton


LONDON, England


NGULI wa zamani wa Mbio za Magari yaendayo kasi Duniani, Langalanga, Ron Dennis amempa nafasi ya kutwaa ubingwa wa 'Formula One' dereva wa Merceds Benz, Lewis Hamilton kutokana na juhudi alizozionyesha kwenye michuano hiyo.


Hamilton alitwaa ubingwa wa Brazilian Grand Prix hivi karibuni baada ya kutoka kwenye majeraha ya goti.

Ron Dennis alisema kuwa anampa nafasi ya kutwaa ubingwa wa Dunia wa Formula One kutokana na juhudi anazoendelea kuzionyesha kwenye mbio mbali mbali za michuano hiyo.
 
Hadi sasa Hamilton ameshashinda kwenye mbio 52 tangu aanze mchezo wa Langa langa lakini anafutiwa na upinzani wa hali ya juu mbele ya dereva mwenzake wa Mercedes, Nico Rosberg.

Rosberg anaiongoza mbio hizo za Ubingwa wa Dunia akiwa na pointi 365 wakati Hamilton akiwa na alama 347 wakati wa tatu akiwa ni Daniel Riccuiardo ambaye ana pointi 342.


Hamilton atakuwa bingwa iwapo tu atashinda michuano ya mwisho huku Rosberg asiposhika kwenye nafasi tatu bora.

MOURINHO KUMNASA DEMBELE

Tags


Mourinho Kumnasa Dembele


MANCHESTER, England


MANCHESTER United inamnyatia kinda wa Celtic ya Scotland, Mousa Dembele ili kuimarisha kikosi chake kwenye kipindi cha msimu wa kiangazi.


Manchester United imefikia hatua hiyo baada ya kinda huyo kuonesha kiwango kikubwa kwenye mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia chini umri wa miaka 21, kinda huyo alifunga bao kwa mpira wa adhabu.

Manchester United imetuma wawakilishi kwenye mazoezi ya Celtic ili kuhakikisha wanapata saini ya kinda huyo kabla ya mwisho wa mwezi huu.


Mashetani hao wekundu wamemtuma Skauti David Friilo kwa ajili ya kuangalia uwezo wa kinda huyo mwenye asili ya Afrika.


Chanzo cha habari kutoka England kimesema kuwa Dembele anatarajia kuanza mazungumzo na Manchester United hivi karibuni kwa ajili ya uhamisho wa dirisha dogo la usajili mwezi Januari mwakani.

Mourinho amemfananisha kinda huyo na Straika wake wa zamani Didier Drogba kutokana na aina yake ya uchezaji akiwa uwanjani.

Mchezaji huyo ana thamani ya pauni milioni tano kutokana na kiwango chake kuongezeka siku hadi siku.

Mashetani hao wekundu wa jiji la Machester wanahitaji saini ya kinda huyo ili kuziba nafasi ya Mholanzi Memphis Depay anayetarajia kuondoka kwa mkopo kwenye klabu ya Everton.

Wednesday, November 16, 2016

OKWI ATUA SIMBA

Tags

MSHAMBULIAJI wa zamani wa timu ya Simba na kipenzi cha mashabiki wengi wa wekundu hao, Emmanuel Okwi, amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuitumikia klabu ya Simba.

Habari za ndani zilizopatiklana jana, Mshambuliaji huyo ataanza kuonekana katika mazoezi ya timu hiyo kujiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Huu utakuwa ni msimu  wa tatu tofauti wa Okwi kuichezea Simba  ambapo mara ya mwisho Simba ilimuuza mshambuliaji huyo kwa dau kubwa katika klabu ya Etoile du Sahel ya nchini Tunisia.

Okwi alianza kuichezea Simba mwaka 2009 hadi 2012 na kuondoka kutimkia kwenye klabu ya Etoile Du Sahel ya nchini Tunisia, akarejea tena msimu wa 2013/2014 na kusaini mkataba wa miaka miwili na klabu ya Yanga na alidumu kwa kipindi cha nusu msimu kabla ya kurejea tena Simba.

Msimu wa 2014/2015, Okwi akiwa Simba alicheza nusu msimu kabla ya klabu hiyo kumuuza kwenye klabu ya Sonderjsky ya nchini Denmark ambako hakupata mafanikio na timu hiyo na sasa ameamua kurejea tena kwa wekundu hao.
 
Akizungumzia juu ya kurejea kwa mshambuliaji huyo, Mwenyekiti  wa Kamati ya Usajili ya Klabu ya Simba, Zacharia Hanspope, alisema usajili wa Okwi umekamilika kwa asilimia 80 lakini tayari gaazeti hili lina taarifa kuwa mshambuliaji huyo ameshasaini mwaka mmoja kuitumikia timu hiyo.

 Alisema Simba ina uwezo wa kumleta mshambuliaji yoyote na kwamba sio kwamba wanashindwa kumleta straika mwingine tofauti na Okwi, wanalazimika kumrejesha kwakuwa ni mzoefu wa ligi ya Tanzania tayari alishawahi kuchezea katika klabu za Simba na Yanga.


karate yanoga

Tags

Karate yanoga


NA ABDUL DUNIA


CHAMA cha Karate Tanzania (TASHOKA),
kinatarajia kuandaa mashindano ya kuwasaka mabingwa wa mchezo huo ambao wataiwakilisha nchi kwenye michuano ya kimataifa.

Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu na yatahusisha washiriki kutoka kila pande ya Tanzania.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa TASHOKA, Sensei Rwezaula, alisema kuwa watahakikisha wanaendesha mashindano hayo kwa misingi na katiba ya mchezo huo nchini.

Alisema watachagua mshindi aliyekuwa sahihi ili kupata bingwa atakayeiwakilisha nchini vizuri.

Aidha, Mwenyekiti huyo alisema kuwa watahakikisha wanatembea Tanzania nzima kwa ajili ya kutafuta vijana ambao wanaupenda mchezo wa Karate ili kuibua vipaji hivyo.

Rwezaula amewataka vijana kuupenda mchezo hio ili kuiwakilisha nchi kwenye mapambano ya kimataifa.

"Tunatarajia kuandaa mashindano ya Karate mwishoni mwa mwaka huu ili kupata wapambanaji watakaoweza kushiriki vema mapambano ya Taifa na Kimataifa kwa lengo la kuendeleza mchezo huo," alisema Rwezaula.

TASHOKA imepewa mamlaka na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), linakikisha inaendesha mchezo huo kwa misingi ya katiba ya nchi ili kuibua vijana wenye vipaji vya mchezo wa Karate.

MILAMBO YAN'ARA MWANZA

Tags


Milambo yang'ara Mwanza


NA ABDUL DUNIA


BENDI ya Milambo ya Mwanza imeibuka mshindi wa mashindano ya kumsaka mkali wa muziki wa kizazi kipya (Bongo fleva) kwenye mkoa wa Mwanza.

Bendi hiyo inayohusisha wanamuziki wanne imeibuka kidedea baada ya kutangazwa mshindi wa mashindano hayo, jana mkoani humo.

Wanamuziki wanaounda bendi hiyo ni Rafael Yusto, William Simon 'Mr Champion', Almasi Salum na Vicent Zakaria Vice.

Akizungumza kwa njia ya simu jana, Meneja wa bendi hiyo, Hidaya Milambo alisema kuwa bendi yake ilistahili kupata ushindi huo bnaada ya kujifua kwa muda mrefu.

Alisema kuwa bendi yake ilifanya mazoezi kwa juhudi na ndio maana ikaibuka mshindi wa mashindano ya mkali wa bongo fleva mkoani Mwanza.

Aidha, Meneja huyo alisema kuwa vijana wake wamepania kufanya vizuri kwenye muziki wa Bongo fleva ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Hidaya Milambo amewataka mashabiki wa muziki wa bongo fleva kuiunga mkono bendi hiyo.

"Tunashukuru kwa kuwa tumepata ushindi wa mashindano ya mkali wa Bongo Fleva, tulistahili kushinda kwa kuwa tulijiandaa vema kuwakabili wapinzani wetu," alisema Meneja wa bendi hiyo.

Baada ya bendi hiyo kuibuka mshindi wa mashindano hayo walipata zawadi ya shilingi mil. 2 na laki tano kutoka kwa baadhi ya wadau wa muziki mkoani Mwanza.

Pia wadau mbali mbali wa muziki wa bongo fleva Mkoani humo waliahidi kuwasaidia vijana hao ili kufikia ndoto zao.

NYOTA AZAM ANOGEWA

Tags


Mghana Azam Anogewa


NA ABDUL DUNIA


STRAIKA mpya wa Azam FC , Samuel Afful amesema kuwa anafurahia kucheza soka nchi Tanzania kutokana na changamoto ya namba aliyokutana nayo.

Straika huyo Mghana ambaye alikuja kwa ajili ya majaribio kwenye Klabu ya Azam FC kwa sasa ameonekana kukubalika na mashabiki na viongozi wa Azam FC kutokana na soka bora alilolionyesha  Juzi.

Mghana huyo alionyesha soka la aina yake kwenye Uwanja wa Azam Complex juzi kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Ruvu Shooting, Azam ilishinda 3-1 huku Afful akitupia moja.

Akizungumza Dar es Salaam, Samuel Afful, alisema kuwa ingawa ni mara yake ya kwanza kucheza Tanzania lakini amekumbana na changamoto ya ushindani kwenye kikosi hicho za Kocha Zeben Hernandez.

Afful alisema kuwa soka la Tanzania lina ushindani kuliko Ghana ambapo kwa kuwa kila timu inahitaji ushindi inapokutana.

"Mpira wa Tanzania una ushindani kuliko kwetu (Ghana) kwa kuwa kila timu ianahitaji ushindi lakini kwetu timu za usgindi zinajulikana mara kwa mara, mpira wa Tanzania uko juu," alisema Afful.

Straika huyo ametua wiki iliyopita akitokea Hasaacas ya Ghana ambapo alikuja na mchezaji mwenzake Agyei Attah kutoka Medeama aliyesajiliwa na Azam FC tangu msimu uliopita.

Sunday, November 13, 2016

habari za michezo

Tags
Penina kidedea Muungano

NA MWANDISHI WETU

MCHEZAJI wa timu ya netiboli ya Jeshi Stars, Penina Mayunga amekuwa mchezaji bora wa michuano ya netiboli kombe la Muungano iliyomalizika juzi jioni viwanja vya Sigara Dar es Salaam.
Michuano hiyo iliyoshirikisha timu nne kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ilikuwa na msisimko mkubwa na timu ya Uhamiaji kutwaa ubingwa wa michuano hiyo.
Uhamiaji ilitwaa ubingwa huo baada ya kuifunga Polisi Morogoro kwa jumla ya mabao 44-35 katika mchezo wa fainali ulioonekana kuwa mkali na ushindani.
Akizungumza Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) Anna Kibira alisema baada ya fainali hiyo kamati ya ufundi ya michuano hiyo ilikaa na kuchambua wachezaji waliofanya vema  tangu michuano hiyo ianze na kuona Penina alistahili kuwa mchezaji bora wa michuano hiyo.
Alisema licha ya timu yake kutocheza fainali, mchezaji huyo alionesha nidhamu ya mchezo kuanzia mchezo wa kwanza hadi hatua ya nusu fainali hatua iliyowavutia viongozi na hata kamati ya mashindano hayo.
"Baada ya michuano kumalizika kamati ya ufundi ilitoa orodha ya wachezaji ambao wamefanya vema tangu michuano ya kombe la muungano ianze ambapo Penina ndeye mchezaji aliyeonekana kuwazidi wachezaji wenzake kwa kuongoza kufanya vema ikiwemo nidhamu ndaangu mwanzo hadi mwisho wa michuano,"alisema Kibira.
Alisema michuano hiyo imekuwa ikiwaunganisha pamoja na kudumisha uhusiano baina ya Tanzania Bara na Zanzibar hali inayosababisha kufanya michuano hiyo kila mwaka kwa mfumo wa kupokezana.
"Mwakani michuano hii itafanyika Zanzibar na timu za Tanzania Bara zitapata fursa ya kusafiri kuwafuata wenzetu hivyo tunamshukuru mungu kwa mwaka huu kuweza kutusaidia kumaliza salama michuano hii,"alisema Kibira.
Alisema bingwa wa michuano hiyo anabaki kuwa bingwa lakini hakuna nafasi ya kuwakilisha nchi katika michuano ya kimataifa isipokuwa bingwa wa michuano ya klabu bingwa Tanzania ndiye anayepata nafasi ya kucheza michuano ya Afrika Mashariki ambapo timu hiyo hiyo ya Uhamiaji ndiyo iliyotwaa pia kikombe cha ubingwa wa klabu bingwa Tanzania michuano iliyofanyika mapema mwaka huu mjini Dodoma.

Mwisho
@@@@@@@@

Yanga kutimkia Ulaya

NA MWANDISHI WETU
UONGOZI wa Yanga upo kwenye mipango ya mwisho kuipeleka timu hiyo kupiga kambi barani Ulaya ili iweze kujipanga vema kwa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na michuano ya Klabu Bingwa Afrika.
Yanga imemaliza mzunguko kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara ikiwa na pointi 32 nyuma ya vinara wa timu hiyo Simba ambayo ina pointi 35 baada ya mechi 15 kwa kila mmoja.
Yanga imefikisha pointi hizo baada ya kushinda michezo 11, ikifungwa michezo miwili  na kutoka sare michezo miwili .
Yanga mwakani itacheza michuano ya klabu Bingwa Afrika, huku Azam ikiwakilisha nchi kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika michuano ya klabu bingwa kwa mwaka huu, Yanga ilishia hatua ya 16 bora , na kufanikiwa kutinga hatua ya Makundi ya kombe la Shirikisho Afrika ambayo ilimaliza katika kundi A ikiwa nafasi ya nne kwenye kundi lililokuwa na timu Kama TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mo Bejaia ya Algeria na Madeama ya Ghana.
Akizungumza Dar es Salaam jana, mmoja wa viongozi wa Yanga, alisema mipango iliyopo sasa ni kutafuta kambi tulivu kwa timu yao ambayo wamepanga iende barani Ulaya.
Alisema wanatambua changamoto na ushindani mkubwa uliopo kwenye ligi msimu huu lakini pia ugumu wa michuano ya kimataifa hivyo wanataka kujiimarisha kabla ya muda kufika.
"Tupo kwenye mipango ya kuona kambi itawekwa nchi gani , lakini hasa hasa barani Ulaya, baada ya mipango kukamilika tutawafahamisa itakuwa ni nchi gani,"alisema kiongozi huyo.
Yanga inadaiwa itapiga kambi nje ya nchi ikiwa na benchi jipya la ufundi chini ya  kocha Mzambia George Lwandamina atakayekuwa akisaidiwa na Charles Boniface Mkwasa na Manyika Peter kocha wa makipa.
Kocha huyo atatua na baadhi ya nyota wake  wa kigeni ambapo baadhi ya wachezaji wa kigeni waliopo sasa wapo watakaoachwa na wengine kutolewa kwa mkopo.
Hata hivyo  hadi sasa Yanga bado haijaweka wazi juu ya maamuzi hayo ya kulitengua benchi lote la ufundi kutokana na kutokuwa na msemaji wa moja kwa moja kulizungumzia suala hilo.
Lakini habari za uhakika ni kwamba tayari  Lwandamina amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia timu hiyo kuanzia mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

@@@@@@@

Yoso 17 wapeta Azam


NA ABDUL DUNIA


VIJANA saba wenye umri chini ya miaka 17, wamepenya kwenye majaribio ya wazi ya mwisho katika mkoa wa Dar es Salaam, yaliyoendeshwa na Klabu Azam
Huo ni mwendelezo wa mpango wa kutengeneza timu bora ya vijana wa umri huo kwa ajili ya kuwatumia kwa miaka ijayo na wengine kunufaika nao kwa kuwauza.
Katika majaribio hayo yaliyofanyika juzi uwanja wa Azam Complex Chamazi Dar es Salaam, vijana 433 wenye umri tofauti kuanzia chini ya umri wa miaka 10, 12, 14 na 17 walijitokeza, ambapo waliweza kuchaguliwa saba na wengine 33 kuorodheshwa.
Mpaka sasa mpango huo umeshahusisha mikoa mitano ikiwemo Dar es Salaam, Tanga, Morogoro, Dodoma na Visiwani Zanzibar, ambako kote kumefanya idadi ya vijana waliofanyiwa usaili kufikia 2,593, kati ya hao 50 pekee ndio waliochaguliwa kushiriki fainali ya mwisho itakayofanyika Uwanja wa Azam Complex mwezi ujao.
Mbali na hao 50, wengine 96 wameorodheshwa na kuhifadhiwa kama akiba ya baadaye.
Taarifa iliyotolewa jana na Mkuu wa Maendeleo ya Soka la Vijana Azam FC, Tom Legg, alisema kuwa amefurashishwa na vijana waliojitokeza kwenye majaribio hayo huku akidai kuwa viwango vilikuwa ni vya hali ya juu.
"Wamejitokeza vijana wadogo sana wanaotoka maeneo ya Chamazi na Mbagala, nimefurahishwa sana kuwaona viwango vilikuwa juu na kiukweli ilikuwa nji nzuri ya kumaliza majaribio Dar es Salaam," alisema.
Alisema kuwa mara baada ya kumaliza vema zoezi hilo Dar es Salaam, hivi sasa mipango iliyopo ni kuthibitisha tarehe za majaribio mengine ya wazi kwenye maeneo yaliyobakia Tanzania.
"Kwa sasa tunachoangalia ni kwenda kwenye maeneo mengine manne kwenye mikoa ya Mbeya, Kigoma, Mwanza na tutahudhuria michuanio ya vijana Arusha Desemba mwaka huu, baada ya hapo katikati ya mwezi Desemba tutafanya fainali ya mwisho hapa Chamazi, ambayo itatoa majibu ya timu yetu ya vijana chini ya umri wa miaka 17," alisema.

Picha za Zile makala

Tags

Picha za zile makala

Mjue Alex Iwobi

Tags
ALEX  IWOBI
 
Kinda la Arsenal linalofananishwa na  Nwanko Kanu.
 
Ni binamu wa Nguli wa Zamani wa Nigeria, Jay Jay Okocha.
 
NA ABDUL DUNIA
 
SOKA ni mchezo namba moja kwa kupendwa duniani.
 
Mchezo huo umejizolea sifa kutokana na aina ya uchezaji wake huku ukiwa umefanya watu wengi kuwa maarufu na kuheshimika.
 
Miongonoi mwa watu ambao wamekuwa maarufu kwa ajili ya soka ni mfalme wa soka duniani Pele, fundi Zinedine Zidane, Ronaldinho, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.
 
Watu hao wamekuwa maarufu sana kutokana na usakataji wao mzuri wa mchezo huo wakiwa uwanjani.
 
Kuna watu ambao walitokea kwenye bara la Afrika na walifanikiwa kufuta tabia za wazungu ambao walikuwa ni wabaguzi wa rangi  kutokana na usakataji wao bora wa soka.
 
Roger Milla, Nwanko Kanu, Samuel Etoo, George Weah na Didier Drogba wameweza kuzibadilisha hisia za wazungu kwenye ubaguzi wa rangi kutokana na uchezaji wao wa mchezo huo.
 
Wachezaji hao waliweza kuheshimika sana na mashabiki wa ulaya na wengine walitengenezewa hadi masanamu kwenye timu zao kutokana na kuhesimika kwao.
 
Uzuri wa mchezo wa soka hauangalii  mwili wala ukubwa wa umri wa mtu hivyo ni mchezo unaotumia akili nyingi kuliko nguvu.
 
Kwa kipindi hiki kuna makinda yanayowika ligi kuu England (EPL) wenye asili ya Afrika.

Alex Iwobi ni mmoja wa makinda kutoka Afrika ambaye amekuwa mwiba kwenye Ligi hiyo.
Kinda wa Arsenal Alex Iwobi alizaliwa may 3, 1996 kwenye mji wa Lagos nchini Nigeria.
Ni mchezaji wa pili kwenye familia yake baada ya binamu yake nguli wa zamani wa Nigeria na klabu ya Fulham ya England Jay Jay Okocha.
Iwobi anacheza nafasi ya winga na mshambuliaji wa kati ambaye amekuwa akiiwakilisha vizuri Nigeria nchini England kwa kipaji chake anachokionesha.
Maisha yake
Iwobi alizaliwa Lagos kabla ya kwenda England akiwa na umri wa miaka minne.
Ambapo alianza soka akiwa kwenye kituo maalum cha soka jijini humo nchini Nigeria.
Safari yake kwenye Soka
Iwobi alijiunga na Arsenal wakati akiwa anasoma shule ya msingi jijini London.
Alijumuishwa kwenye kikosi cha kwanza kama mchezaji asiyetumika wakati akiwa na umri wa miaka kumi na saba kwenye kombe la Ligi dhidi ya West Bromwich Albion Oktoba 25, 2013.
Alisaini mkataba wa muda mrefu akiwa na Arsenal Oktoba 2015 kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo inayonolewa na Kocha Profesa Arsenal Wenger.
Msimu wa 2015-2016
Oktoba 23, mwaka 2015, Iwobi aliingia kwenye kikosi cha kwanza cha Arsenal Wenger kwenye mchezo wa kombe la Ligi mzunguko wa 16 bora dhidi ya Sheffield Wednesday Siku nne baadae alicheza kwa mara ya kwanza Ligi kuu England kwenye ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Swansea City kwenye uwanja wa Liberty chini Wales akichukua nafasi ya Mesut Ozil kwenye dakika ya 85.
Tunaweza kusema kuwa Iwobi kama alikuwa na bahati na Arsenal baada ya kuingia kwenye mchezo wa Ligi ya mabingwa dhidi ya Bayern Munich waliochapwa 5-1.
Baada ya kuanza kwenye kikosi cha kwanza kwenye mchzo dhidi ya Barcelona, kinda huyo alionesha kiwango cha hali ya juu kilichowaduwaza wachambuzi wengi wa soka barani ulaya.
Kinda huyo alianza kucheka na nyavu kwenye mchezo dhidi ya Everton na Watford.
Mashabiki walimbeza
Mashabiki wa Arsenal nchini England walijaribu kumlalamikia kocha wa kikosi hicho Arsenal Wenger kutokana na kumuamini kwake kinda huyo na kujaribu kumuingiza kwenye michezo migumu ikiwemo ule dhidi ya Bayern Munich na Barcelona ambayo yote Arsenal walipoteza.
Aanza Kukubalika
Kutokana na kipaji ambacho Iwsobi alikuwa anakionesha kwenye kila mchezo mashabiki wa Arsenal walianza kuvutiwa na huduma ya kinda ahuyo.
Kinda huyo aliendelea kuwika na Arsenal kwenye msimu uliopita ambapo alikuwa chachu kubwa ya ushindi wa kikosi hicho chenye maskani yake jijini London.
Afananishwa na Mkongwe Kanu
Binamu huyo wa Jay Jay Okocha amewahi kufananishwa na mkongwe wa zamani wa timu ya taifa ya Nigeria na klabu ya Arsenal, Nwanko Kanu kutokana na aina ya uchezaji wanaocheza.
Mashabiki wa Arsenal walimlazimisha Kocha walijaribu kumshawishi Arsenal Wenger kum,patia nafasi ya kudumu kwenye kikosi hicho kinda huyo kwa kuwa anaonesha kiwango kikubwa kuliko mshambuliaji wa timu hiyo, Olivier Giroud.
Atakata dhidi ya Chelsea
Kwenye mchezo uliopigwa hivi karibuni dhidi ya Chelsea, Arsenal ilishinda 3-0, Iwobi alionesha kiwango cha hali ya juu kilichowafanya mashabiki wengi kumshangilia huku wachambuzi wakimsifia kwa ubora wake aliokuwa nao kwenye soka.
Baada ya mchezo huo kumalizika chama cha soka England (FA), kilmzawadia kinda huyo tuzo ya mcheazji bora chipukizi wa mechi.
Timu ya Taifa
Baada ya kucheza timu ya taifa ya vijana kwenye timu ya England, Iwobi alichagua kucheza kwenye timu ya taifa ya Nigeria ambapo alipozaliwa.
Mchezo wake wa kwanza kwenye ti mu ya taifa ya Nigeria ulikuwa dhidi ya DR Congo Ocktoba 8, 2015 alichukua nafasi ya Ahmed Mussa kwenye dakika ya 57. 
Alichaguliwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Nigeria kilichoshiriki michuano ya Olimpiki jijini Rio de Janeiro, Brazil mwaka huu.
England wamgombania
Kabla ya kuamua kuchezea Nigeria, Iwobi alilazimishwa na kocha wa zamani wa England, Roy Hodgson kuwa akubali kujiunga na timu yake ya taifa lakini jitihada za kumshawishi zxiligonga mwamba baada ya kinda huyo kukubali kucheza Nigeria.

huyu ndiye Eric Dier

Tags
ERIC DIER:
 
L Mtoto wa mcheza Tenisi anayemweka benchi Wayne Rooney, England
 
Aliwahi kutesa na Sporting CP ya Ureno, sasa yuko Spurs
 
LONDON, England
 
LIGI Kuu ya England (EPL) ni Ligi yenye msisimko, ushindani na changamoto ya hali ya juu.
 
 
Hiyo yote  ni kutokana na timu mbalimbali zilivyoweza kujiandaa wakati wa maandalizi yake ya usajili kwa ujumla ili kujiweka fiti kwa michuano hiyo.
 
Miaka mitano iliyopita Ligi hiyo ilikuwa ngumu, tamu na aina yake kwa kuwa ilisheheni wachezaji mbalimbali wenye nguvu na uwezo wa kusakata kabumbu.
Kuna waliopita akina Benjamin Mwaluwali, Benny Mcarthy, Emmanuel Adebayor, Paul Schoels na wengine ambao walikuwa wakiongeza radha ya Ligi.
 
 
Walikuwepo watukutu akina Roy Keane, Patric Viera, Joey Barton na Michael Barack lakini sasa hawapo.
 
 
Kuondoka kwa mafundi na watukutu England kumechangia kwa kiasi kikubwa kuporomoka thamani halisi ya EPL.
 
 
Lakini sasa kuna wachezaji ambao wanakipiga EPL kwenye vilabu tofauti tofauti unaweza kujaribu kuwafananisha na mafundi wale walioondoka England.
 
 
Ndio, unaweza kuhisi kuwa utamu wa EPL miaka mitano iliyopita unarejea tena kutokana na baadhi ya wachezaji kufanya kweli kama wakongwe waliopita.
 
 
Wapo akina Mesut Ozili, Paul Pogba, Diego Costa, Sadio Mane na wengineo.
Lakini Uhuru Jumatatu, limekuandalia makala haya ili kukueleza maisha ya Kiraka Eric Dier anavyoifanya EPL kurejea kwenye utamu wake.
 
 
Ndio Dier ni mchezaji mwenye kiwango bora kwa sasa England ambaye amekuwa akiwakumbusha mashabiki wa Ligi hiyo duniani enzi za akina Xabi Alonso na Claudio Makelele.
 
 
Huyu ndiye Dier
 
Anaitwa Eric Jeremy Edger Dier,  alizaliwa January 15 1994 kwenye jiji London nchini England.
 
Ni mwanasoka raia wa England anayekipiga Ligi Kuu England kwenye klabu ya Tottenham Hotspur pamoja na timu ya taifa ya England.
 
Alizaliwa kwenye kitongoji kidogo cha Cheltenham jijini Gloucedstershire nchini England.
 
 
Dier alihamia nchini Portugal na familia yake kipindi akiwa na umri wa miaka saba kutokana na Mama yake kupata kazi ya kuhudumia wachezaji uwanjani kwenye michuano ya Ulaya (UEFA EURO) iliyofanyika Ureno.
 
 
Dier aliishi mwaka mmoja katika jiji la Algarve kabla ya kuhamia jijini Lisbon kwa ajili ya makazi rasmi na familia yake.
 
 
Mwaka 2010, wazazi wake walirejea England wakati Dier aliendelea kuishi Ureno huku akiwa anaitumikia timu ya vijana ya Sporting CP ya nchini humo.
 
 
Dier ni Mjukuu wa Ted Croker ambaye ni katibu mkuu wa zamani wa Shirikisho la Soka England (FA) rais wa mji mdogo wa Cheltenham.
Vile vile Binamu yake ni Peter Croker ambaye ni mwanasoka wa zamani wa Charlton Athletic.
 
Amkana baba yake, ajiingiza kwenye soka
 
Unaweza kusema kuwa Dier alimkana baba yake kwa kuwa baba yake, Jeremy Dier ni mchezaji mkongwe wa zamani wa mchezo wa Tenisi nchini England.
 
Fundi huyo aliamua kujiingiza kwenye soka wakati akiwa na umri wa miaka saba nchini England wakati baba yake alitaka amrithishe kwenye mchezo wa Tenisi.
 
 
Maisha yake ya Soka
 
Wakati akiwa nchini Portugal Dier, alifanikiwa kuitumikia timu ya soka ya shule aliyokuwa anasoma ambapo alionesha kiwango cha hali ya juu hadi akajumuishwa kwenye timu ya vijana ya Sporting CP nchini humo wakati akiwa na miaka nane.
 
 
 
Dier alisaini mkataba wa miaka mitano kwenye klabu ya Sporting mwaka 2010 ili kuitumikia kwenye michuano mbali mbali ya ulaya.
 
 
Wakati Dier alipokuwa akiichezea Sporting, timu hiyo iliweza kuzifunga timu kongwe za England ambazo ni Arsenal, Tottenham Hotspur na timu aliyokuwa akiishabikia Dier wakati akiwa mtoto mdogo, Manchester United.
 
 
Mnamo January 2011, Dier alikubali kujiunga na Everton kwa mkopo.
 
Alipokuwa Everton kwa mkopo Dier alikuwa akicheza kikosi cha chini ya miaka 18 kutokana na umri wake kutomruhusu mkucheza timu ya wakubwa.
 
 
Dier na wenzake waliweza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu England chini ya miaka 18 kwenye msimu wa 2010- 2011.
 
 
Novemba 4 2012, Dier alifunga bao lake la kwanza akiwa na kikosi chake cha Sporting kwa mkwaju wa adhabu ndogo dhidi ya Benfica B.
 
 
Aitwa kikosi cha wakubwa
 
 
Novemba 11 2012, Dier alicheza mchezo wake wa kwanza na kikosi cha timu ya wakubwa Sporting CP akichukua nafasi ya Ricky van Wolfswinkel kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Ureno dhidi ya Braga.
 
 
Siku kumi na tano baadae, Dier alifunga bao lake la kwanza kwenye mchezo wa Ligi dhidi ya Moreirense ugenini wakati timu yake ikitoka sare ya mabao 2-2.
 
 
 
Atimkia Spurs
 
Agosti 2 mwaka 2014, Dier alisaini mkataba wa miaka mitano katika klabu ya Tottenham Hotspur kwa ada ya Pauni milioni 4.
 
Mashabiki wa Spurs haweakuamini kuwa Dier anaweza kutakata na kumnyima namba kiungo mkongwe wa zamani wa klabu hiyo Mualgeria Nabil Bentalleb kutokana na kiwango chake.
 
 
Mchezo wake wa kwanza kucheza akiwa na Spurs ulikuwa dhidi ya West Ham United kwenye msim u wa mwaka 2014-2015 ambapo alifunga bao pekee katika dakika za nyongeza.
 
Dier alianza kwenye kikosi cha kwanza March 1 mwaka 2015 ambapo Spurs ilifungwa 2-1 dhidi ya Chelsea kwenye mchezo wa fainali ya kombe la Ligi kwenye dimba la Wembley.
 
 
Dier alisaini mkataba mpya Septemba 9 mwaka jana wa kuitums hadi 2020.
 
Dier alianza kuaminiwa na kocha wa kikosi hicho Mauricio Pochettino ambapo alikmuwa akimuanzisha nafasi ya kiungo mkabaji.
Septemba 13 mwaka huu, Dier alisaini mkataa mpya utakaoweza kumbakisha Spurs hadi mwaka 2021.
 
 
Timu ya taifa ya England
 
Dier alianza kuitumikia timu yake ya taifa ya England chini ya umri wa miaka 19 mwaka 2012.
Shirikisho la Soka nchini Ureno kuitumikia Ureno lakini ilishindikana kutokana na mchezaji huyo kuwa mzalendo na nchi yake.
 
 
 
Dier alifunga bao lake la kwanza kwenye kikosi cha timu ya taifa ya chini ya umri wa miaka 18 baada ya Kocha wa kikosi hicho cha 'Three Lions' kumuanzisha kwenye mchezo dhidi ya Slovakia.
 
Baada ya kiwango chake kuimarika zaidi ya awali kocha wa kikosi cha England chini ya 21, Peter Tylor alimjumuisha kwenye kikosi chake kilichoshirikmi Kombe la Dunia mwaka 2013.
 
 
Kutokana na kucheza nafasi zaidi ya moja uwanjani Kocha wa kipindi hiko wa England alimtumia kama beki wa kulia kwenye kikosi hicho.
 
Novemba mwaka jana, Dier alichaguliwa kwenye kikosi cha wakubwa cha England na Kocha wa zamani Roy Hodgson kwa ajili ha mchezo wa kirafiki dhidi ya Hispania na Ufaransa.
 
Dier alianza kwenye mchezo dhidi ya Ufaransa uliochezwa kwenye uwanja wa Wembley ambapo alicheza kwa kiwango cha hali ya juu huku akiibuka mchezaji bora wa mchezo huo.
 
Alifunga bao lake la kwanza kwenyew timu ya taifa ya England mnamo March 2016, kwenye mchezo wa kirafiki dhidi ya Ujerumani.
 
 
Dier aliitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya England kilichokwenda Ufaransa kucheza michuano ya Ulaya (UEFA EURO).
 
 
Alifunga bao kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Urusi kwa mkwaju wa adhabu ndogo uliokwenda moja kwa moja nyavuni.
 
Amuweka Rooney Benchi
 
 
Kipindi hiki Dier ndiye anayemweka benchi nahodha wa Kikosi hichi cha 'Three Lions', Wayne Marc Rooney kutokana na kuwa kipenzi cha mashab iki wa England.
 
Dier ni kipenzi cha mashabiki wa England kwa kuwa kiwango chake kina imarika siku hadi siku.
 
Afananishwa na Scholes, Keane
 
Aliweza kufananishwa na mkongwe wa zamani wa England na Manchester United Paul Scholes kutokana na aina ya uchezaji anavyocheza uwanjani.
 
 
Mashabiki wa England wanamfananisha Dier na kiungo mtukutu wa zamani wa Manchester United, Roy Keane kutokana na kulisakata soka vizuri
 
 
Nafasi anazocheza
 
Eric Dier ni kiraka kwa kuwa ana uwezo wa kucheza zaidi ya namba moja uwanjani.
 
 
Ana uwezo wa kucheza nafasi ya Kiungo mkabaji, beki wa kati na beki wa pembeni.